BENKI KUU YA USHIRIKA TANZANIA ''TANZANIA COOPERATIVE BANK......''

 Benki kuu ya Ushirika nchini Tanzania yenye makao yake makuu jijini Dodoma! inatazamiwa kuwa ni mkombozi wa vyama vya Ushirika nchini, Je, ni kweli?

ELIMU NA UMUHIMU WA VYAMA VYA USHIRIKA NCHINI TANZANIA KWA MAENDELEO YA NCHI

Unaposikia neno “USHIRIKA” wengi wetu tunapata picha kwamba ni swala linalowahusu wakulima na ni kwa baadhi ya maeneo fulani tu! Dhana hii si kweli hata kidogo. Ushirika ni mfumo unaowaunganisha jamii fulani kwa hiari yao wenyewe bila kulazimishwa na mtu yeyote ili wawezekuunganisha nguvu zao kwa pamoja katika kutatua changamoto zinazo wakabili kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Mh. raisi, najua unajua umuhimu wa vyama vya ushirika vile vyama vya msingi, vyama vikuu na vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa (saccos). Vyama vya ushirika ni kiunganishi tosha kati ya serikali na wakulima, vikitumika ipasavyo ni rahisi serikali kuwafikia wakulima moja kwa moja na hivyo kuwa rahisi kwa serikali kusimamia miradi yake kwa wananchi. Lakini pia vyama vya ushirika moja ya kazi zake ni kutafuta masoko ya vinavyo zalishwa na wanachama wake, ni vigumu sana kwa mkulima peke yake kupata soko la uhakika kulinganisha  na akiwa kwenye chama cha ushirika. Mkulima peke yake ni ngumu sana kushindana sokoni kutokana na uhalisia wa dunia ya leo yenye teknolojia inayokua kila kukicha. Kuna vyama vya ushirika mazoa vya kahawa, pamba, mkonge tuliona jinsi vilivyo kuwa na nguvu kiuchumi, vyama kama kama Kilimanjaro Native Cooperative Union (KNCU), Nyanza Cooperative Union (1984) Limited (NCU), Coastal Region Cooperative Union (CORECU), Morogoro Region Cooperative Union n.k, lakini pia tunaweza kuanzisha vyama vya ushirika kwa wakulima wa miwa kwenye viwanda vya sukari, wakulima wa mpunga, wakulima wa korosho, wakulima wa mbaazi, wakulima wa vitunguu, wakulima wa nyanya, wakulima wa maharage, dengu, wafugaji n.k

Mh.raisi, faida za kuwa na vyama imara vya ushirika ni nyingi zikiwemo zifuatazo;

  1. Fursa za ajira. Vyama vya ushirika ni chanzo kikubwa cha uhakika cha kutoa ajira, kuna maafisa ushirika wilaya, mkoa, kanda, wasimamizi wa vyama vya ushirika, mameneja wa vyama vya ushirika, wahasibu wa vyama vya ushirika, washauri wa vyama vya ushirika, maafisa mipango wa vyama vya ushirika n.k

Chuo cha ushirika kinazalisha wataalamu wengi sana katika fani ya usimamizi wa vyama vya ushirika kila mwaka lakini matunda yake hayatumiki ipasavyo sababu hakuna pa kuwapeleka na mwisho wa siku itaonekana kozi zinazohusu ushirika hazina tija teja nchini Tanzania wakati sio kweli, Tanzania tunahitaji ushirika kwa kiasi kikubwa sana kutokana na mazingira yetu yalivyo. Watu wanapo zungumzia ushirika wanajua moja kwa moja ni kilimo tu! Dhana hii sio kweli kabisa, ushirika upo kwenye kila nyanja, miaka ya karibuni kumekuwepo na wajasiriamali wengi sana wadogo ambao kwa mmoja mmoja imekuwa ngumu kufikia soko la kikanda lakini kupitia ushirika tungeweza kufikia soko hilo kwa urahisi zaidi. Wajasiriamali wanatengeneza sabuni za miche, sabuni za maji, madawa ya kusafishi vyoo, pilipili, penunt butter, viungo vya chai, nguo, viatu, wanafuga kuku wa mayai na kuku wanyama n.k Kama wasomi kwenye fani ya ushirika tungepewa nafasi ya kuwafikia na kufundisha elimu hii kwenye jamii basi si ajabu leo hii tungekuwa tuna vyama vya ushirika vya watengeneza nguo, vyama vya ushirika vya wategeneza viatu, vyama vya ushirika vya wasindikaji wa vyakula, vyama vya ushirika vya wafuga kuku n.k

VYAMA VYA USHIRIKA NI SULUHISHO LA UPATIKANAJI WA MASOKO KWA WAKULIMA NA WAFUGAJI TANZANIA

Unaposikia neno “USHIRIKA” wengi wetu tunapata picha kwamba ni swala linalowahusu wakulima na ni kwa baadhi ya maeneo fulani tu! Dhana hii si kweli hata kidogo. Ushirika ni mfumo unaowaunganisha jamii fulani kwa hiari yao wenyewe bila kulazimishwa na mtu yeyote ili wawezekuunganisha nguvu zao kwa pamoja katika kutatua changamoto zinazo wakabili kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Vyama vya ushirika ni kiunganishi tosha kati ya serikali, wafanya biashara na wakulima vikitumika ipasavyo ni rahisi serikali kuwafikia wakulima moja kwa moja kusimamia miradi yake kwa wananchi lakini pia wakulima kuwafikia wasambazaji wa pembejeo na wateja. Moja ya kazi za vyama vya ushirika ni kutafuta masoko kwa wakulima na wafugaji, ni vigumu sana kwa mkulima ama mfugaji wa Tanzania mmoja mmojan kufikia soko la uhakika kulinganisha  na wakiwa kwenye chama cha ushirika. Mkulima peke yake ni ngumu sana kushindana sokoni kutokana na uhalisia wa dunia ya leo yenye teknolojia inayokua kila kukicha na udhaifu wa uchumi wake binafsi. Kuna vyama vya ushirika vya mazoa ya kahawa, pamba, mkonge tuliona jinsi vilivyo kuwa na nguvu kiuchumi, vyama kama Kilimanjaro Native Cooperative Union (KNCU), Nyanza Cooperative Union (1984) Limited (NCU), Coastal Region Cooperative Union (CORECU), Morogoro Region Cooperative Union n.k, lakini pia tunaweza kuanzisha vyama vya ushirika kwa wakulima wa miwa kwenye viwanda vya sukari, wakulima wa mpunga, wakulima wa korosho, wakulima wa mbaazi, wakulima wa vitunguu, wakulima wa nyanya, wakulima wa maharage, dengu, wafugaji na wajasiriamali wetu.

Tanzania ipo kwenye ukanda wa jumuia ya Afrika Mashariki ambapo tuna soko la pamoja, wakulima, wafugaji na wajasiriamali wetu imekuwa ni vigumu kupenya kwenye soko kutokana na wengi wao kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya kuyafikia masoko husika, hii inatoa mwanya kwa wajanja wachache kunufaika na kuwaacha wakulima na wajasiriamali wadogo wakiwa hawana la kufanya. Hali hii inasababisha mambo mengi kutokea ikiwemo watu wa kati kuingilia kwa madai ya kuwasaidia wakulima wakati kiuhalisia wana wanyonya wakulima, taasisi mbalimbali kuingilia kwa lengo la kuwasaidia wakulima hali ya kuwa sio kweli!

Pongezi kwa taasisi ya SIDO inafanya jitihada kubwa sana katika kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa watanzania wengi na ukweli ni kwamba elimu hiyo imewasaidia watanzania wengi wamekuwa wajasiriamali changamoto pekee ni namna ya kupata soko la ndani na nje ya nchi na hapa ndipo umuhimu wa kuwa na vyama vya ushirika unapokuja na kuwa mkombozi pekee wa kuwapatia masoko kwa kuwa na wataalamu wabobezi. Swala la wakulima na wajasiriamali kukosa masoko kwa bidhaa zao inaweza kupungua na/au kuisha kabisa kama serikali ikiweka kipaumbele na mipango mikakati madhubuti kupitia wizara ya ushirika na kilimo kutoa elimu ya vyama vya ushirika na kuvisimamia ipasavyo ili kuleta tija. Tuna vijana wengi wabobezi kutoka chuo pekee kinachotoa mafunzo ya vyama vya ushirika kwa ngazi za cheti, diploma na digrii ukanda wote wa Afrika Mashariki na kati, Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), ili kusaidia kuwa na vyama vya ushirika imara na vyenye nguvu kuwatetea wakulima, wafugaji, wajasiriamali na watu wa kada maalumu katika kufikia fursa za masoko ndani na nje ya nchi.

Kuna nchi  nyingi zilizo tuzunguka ambao wana uhitaji mkubwa wa vyakula kama mahindi. Baadhi ya nchi kama vile Sudani na Somalia wanauhitaji mkubwa wa mahindi lakini imekuwa changamoto kwa wakulima na wafugaji wetu kufikia hili soko. Nchi jirani kama Kenya wanatumia fursa hii ya kuchukua mazao utoka Tanzania na kufikisha kwenye hizi nchi hali ya kuwa wakulima wetu wanashindwa kupata maendeleo stahiki.

Nchi yetu ina utajiri wa mazao kama vile mahindi, vitunguu, nyanya, ndizi, maparachichi, mbaazi, miwa, pamba, korosho, dengu n.k ikiwekwa mipango thabiti wakulima na wafugaji wetu watapata kufurahia nguvu zao na kuongeza tija katika shughuli zao na hatimaye kuchangia pato la taifa kwa ujumla.


MAANA NA DHANA HALISI YA USHIRIKA


Nini maana ya ushirika......?

“Ushirika”, ni mkusanyiko wa watu walioamua kuungana kwa ridhaa yao wenyewe bila kulazimishwa kwa lengo la kusaidiana kupata mafanikio ya kiuchumi, kijamaa, kitamaduni na mahitaji mengine kupitia umiliki wa pamoja kwa kutumia demokrasia kwa wanachama wote.

Ushirika kama vyama vingine unaendeshwa katika misingi na kanuni zake katika kuhakikisha malengo husika ya ushirika yanatimia. Lakini pia thamani ya ushirika imejengwa kwenye misingi kadha wa kadha.

Thamani ya ushirika inajengwa juu ya kusaidiana wenyewe kwa wenyewe, uwajibikaji wa kila mwanachama, upendo kwa kila mwanachama, demokrasia inayotoa haki sawa kwa wote, kuwa na umoja, usawa na mshikamano. Kwa kuzingatia hayo yote ndipo thamani ya ushirika inapopatikana.

Kanuni za vyama vya ushirika

Ushirika ukiwa kama taasisi ni lazima ziwepo kanuni zitakazotoa muongozo wa namna ushirika unatakiwa uwe ili kufanikisha malengo ya ushirika. Ushirika unaendeshwa kwa kuzingatia kanuni zifuatazo zikiwa kama sheria na muongozo;

Uanachama wa chama cha ushirika upo wazi na kwa kila mtu. Hii ni kanuni ya kwanza kabisa ambayo inatoa fursa kwa kila mtu mwenye akili timamu kuweza kuwa mwanachama wa chama cha ushirika chochote ili mradi aweze kukubaliana na mahitaji ya chama cha ushirika husika. Hii pia inatoa mwanaga kwa watu wa kada zote kwamba dhana ya ushirika inafanyakazi kwa kada zote, hapa namaanisha kunaweza kuwa na vyama vya ushirika vya wafanyakazi, vyama vya wakulima, ushirika wa wafanya biashara n.k

Demokrasia katika kusimamia na kuendeleza chama. Kuna dhana imejitokeza kwamba mtu mmoja anaweza kuanzisha chama cha ushirika na kuratibu kila kitu, hii si sawa hata kidogo! Chama cha ushirika sio taasisi ya mtu binafsi bali ni taasisi ya wanachama kimuundo na kiuendeshaji na kila mwanachama ana haki sawa katika chama! Hakuna aliyekuwa juu ya sheria au juu ya mwenzake. Hali hii inapelekea chama kuwa na amani, usawa, umoja na mshikamano muda wote.

Ushirikishwaji katika kujenga uchumi wa chama. Vyama vya ushirika vinamjenga mwanachama kuweza kujitegemea na kujua njia bora na sahihi za kutengeneza uchumi. Hali hii inatokana na darasa analopata mwanachama katika kujenga uchumi wa chama kwa kuchangia mtaji wa chama lakini pia ushiriki wake katika kusimamia na kuendesha mali za chama.

Uhuru. Chama cha ushirika kipo huru na wanachama wanasaidiana wenyewe kwa wenyewe bila kusubiri msaada wowote na bila masharti yoyote. Inapotokea chama kimelazimika kupata pesa au kuingia mkataba na taasisi yoyote nje ya chama basi zoezi kama hili linafanyika kwa kushirikisha wanachama wote kuwa na maamuzi ya pamoja.

Elimu, Mafunzo na kupeana taarifa baina ya wanachama. Kuwa kwenye chama cha ushirika kuna raha sana, wanachama wanapata fursa ya kupatiwa elimu na mafunzo mbalimbali ya kuwajenga kwa gharama ndogo sana. Wanapatiwa fursa za kuhabarishwa juu ya mambo mbalimbali yanayo endelea, taarifa za masoko, taarifa za uwekezaji n.k, hioi yote inafanyika ni katika kuwajengea wanachama uwezo

Ushirikiano na vyama au taasisi nyingine. Ushirika raha sana! Chama cha ushirika kinampa mwanachama fursa ya kushirikiana na vyama vingine au taasisi nyingine taasisi ambazo kwa mtu mmoja mmoja huenda ingekuwa ni vigumu kushirikiana nazo lakini kupitia ushirika mtu wa wa hali ya chini kabisa ambaye ni mwanachama wa chama cha ushirika anaweza akashirikiana na taasisi au mashirika mengine.

Kuzingatia maendeleo ya jamii. Vyama vya ushirika vinafanyakazi bega kwa bega kuhakikisha jamii inayoizunguka inapata maendeleo kutokana na uwepo wa chama cha ushirika katika maendeieo yao. Hii ni pamoja na kutoa ajira kwa wanajamii na kutoa huduma kwa jamii husika

Yote kwa yote hii inaonyesha ni kwa jinsi gani vyama vya ushirika vilivyokuwa kumuhimu kwenye jamii zetu

BENKI KUU YA USHIRIKA TANZANIA ''TANZANIA COOPERATIVE BANK......''

 Benki kuu ya Ushirika nchini Tanzania yenye makao yake makuu jijini Dodoma! inatazamiwa kuwa ni mkombozi wa vyama vya Ushirika nchini, Je, ...